Sunday 22 February 2015

MBUNGE CANADA ALAUMU KUBANWA NA 'CHUPI'




Mbunge wa Canada alitoa kisingizio cha ajabu kuwahi kutolewa kwa kuondoka bungeni haraka – nguo ya ndani kumbana.

Ilivyoonekana nguo za ndani zilizombana zilimpa ugumu kukaa wakati walipokuwa wakipiga kura, mbunge wa upinzani Pat Martin alimwambia Spika aliyekuwa kamahanika.

Hatahivyo, aliwahi kurudi kupiga kura yake.

Bw Martin alizua vifijo na vicheko bungeni humo baada ya kuelezea sababu za kutoka kwa muda.

"Walikuwa wakiuza chupi za kiume kwa nusu bei na mie nikanunua kadhaa ambazo bila shaka zimekuwa ndogo kwangu. Napata ugumu kukaa kwa hakika.”

Spika wa bunge hilo alisema awali alimwamuru Bw Martin kukaa chini alipotaka kuondoka.

"Sikuelewa ufafanuzi wake wakati huo na sidhani kama naielewa sasa”, alisema.

Chanzo: BBC
Imetafsiriwa na Mwandishi wetu

No comments:

Post a Comment