Sunday 8 February 2015

MASHABIKI WA MPIRA WAZUA GHASIA, 14 WAFARIKI



 Egyptian firefighters extinguish fire from a vehicle outside a sports stadium in a Cairo"s northeast district

Takriban watu 14 wamefariki dunia katika mapambano yaliyozuka baina ya mashabiki wa mpira na polisi nje ya uwanja wa mpira mjini Cairo, chombo cha habari cha taifa cha Misri kimeripoti.

Mashabiki wa klabu ya mpira ya Zamalek walijaribu kuingia uwanjani kutazama mechi bila tiketi, na kuchochea ghasia hizo, maafisa walisema.

Vurugu hizo zilianza kabla ya mechi baina ya pande za Zamalek na ENPPI.

Februari 2012, zaidi ya watu 70 walikufa katika ghasia zilizozuka baada ya mechi huko Port Said.


No comments:

Post a Comment