Wednesday 4 February 2015

KENYA KUPEWA MKOPO WA DOLA MILIONI 700



 IMF Managing Director Christine Lagarde shaking hands with Kenyan president Uhuru Kenyatta. 4 January 2014

Shirika la Fedha duniani IMF  limekubali kutoa mkopo wa takriban dola milioni 700 nchini  Kenya.

Fedha hizo zitatumika kama sera ya bima kujilinda kwa tishio lolote la uchumi wa nchi, ikizingatiwa nchi hiyo iko imara kiuchumi Afrika Mashariki.

Serikali ya Kenya iliomba pesa hizo kama njia ya tahadhari, iwapo kutatokea dharura kama vile majanga ya asili au mashambulio kutoka kwa wapiganaji.

Fedha hizo zitakuwepo kwa kipindi cha miezi 12 ijayo.

Wizara ya fedha imeiambia IMF haina nia ya kutumia pesa hizo.

Badala yake itatumika kama kinga dhidi ya “mtikisiko wa kiuchumi”, IMF ilisema.

Chanzo: BBC
Imetafsiriwa na Mwandishi wetu

                                                                                                        


No comments:

Post a Comment