Friday 27 February 2015

MTOTO ALIYETEKWA APATIKANA BAADA YA MIAKA 17


Celeste Nurse (in orange dress) and her husband Morne (in cardigan) leaving the Cape Town Magistrates Court on 27 Febraury
Celeste Nurse na mumewe Morne wana furaha hatimaye kumpata binti yao

Mwanamke mmoja Afrika kusini amefikishwa mahakamani kwa kumteka mtoto mchanga kwenye hospitali ya Cape Town miaka 17 iliyopita.

Wazazi halisi wa binti huyo, Celeste na Morne Nurse, walikutanishwa naye baada ya kujikuta kaanzishwa shule moja na dada yake.

Baada ya kuona namna walivyofanana, wazazi halisi wa familia hiyo walimwalika binti huyo kupata kahawa na hapo ndipo walipowasiliana na polisi.

Vipimo vya asidi nasaba vimethibitisha utambulisho wa binti huyo, ambaye amepelekwa ustawi wa jamii kwa sasa.

Bw Nurse alisema binti yake anapewa ushauri nasaha wa kina.

Mke wake alisema ni “kama ndoto” kumwona mtoto wake tena.

"Alipokutana na Cassidy [dada yake], kulikuwa na kitu kiliwavuta tu na ikaanzia hapo," aliiambia redio ya CapeTalk.

"Siku yake ya kuzaliwa ni tarehe 28 Aprili. Mwaka huu tunaweza kusherehekea naye. Itakuwa mara yetu ya kwanza naye na lazima tupange kitu kikubwa sana."

Ndugu wa anayedaiwa kumteka aliwaambia waandishi wa habari nje ya mahakama ya Cape Town: 
"Tumekuzwa na binti huyu, tumemtunza."

Mwanamke huyo aliyekamtwa na mumewe, hawana watoto wengine.

Mwanamke huyo, mwenye umri wa miaka 50, anashtakiwa kwa utekaji nyara, udanganyifu na kukiuka sheria ya Watoto, hivyo basi amedanganya kuwa yeye ni mama mzazi wa mtoto huyo, polisi walisema.

Kesi yake imeahirishwa mpaka tarehe 6 Machi.

No comments:

Post a Comment