Sunday 8 February 2015

DEREVA ALIYEFUKUZWA AKUSUDIA KUUA 50


 East Africa bus. (AP)



Polisi nchini Uganda walisema walimkamata dereva aliyejaribu kuligonga basi kwenye mto ulojaa mamba kwa nia ya kuua abiria 50 waliokuwa kwenye chombo hicho baada ya kufukuzwa kazi.

“Tulipojua kuhusu utekajinyara huo, tuliweka vizuizi  kabla ya  mto huo ..tulimvamia halafu tukamkamata.” Alisema Denis Namuwooza,  mkuu wa polisi katika wilaya ya Kasese kusini-magharibi mwa Uganda.

Dereva huyo, ambaye polisi walisema alifukuzwa kutokana na ulevi, iliripotiwa alikusudia kulirusha basi hilo huko Kazinga, mto ambao aghlabu hujaa viboko, ambao huunganisha maziwa mawili makubwa katika mbuga ya wanyama ya Queen Elizabeth nchini Uganda.

Aliwaambia abiria "atakufa pamoja na wao kwa kulirusha basi Kazinga, “ alisema mmoja aliyenusurika, Dinah Mwagale Mudusu, akizungumza na chombo cha habari cha Uganda.

Chanzo: AFP 
Imetafsiriwa na Mwandishi wetu                                                    

No comments:

Post a Comment