Friday 27 February 2015

GAUNI LA LUPITA NYONG'O LA $150,000 LAIBIWA



 

Gauni rasmi lenye thamani ya $150,000 lililoshonwa rasmi na kampuni ya Calvin Klein, na kuvaliwa na muigizaji Lupita Nyong'o wakati wa tuzo za Oscars, limeibiwa Hollywood.

Gauni hilo, lililopambwa na lulu nyeupe 6,000, liliibiwa katika hoteli moja, Nyong'o alipokuwa nje ya chumba chake.

Mkenya huyo alishinda muigizaji msaidizi bora mwaka jana kutokana na filamu ya Twelve Years a Slave na alikuwa miongoni mwa watangazaji katika shughuli ya Jumapili.

Jarida la People limemtaja kuwa mtu mrembo duniani wa mwaka 2014.

Polisi Lt William Nash alisema gauni hilo linaonekana kuibiwa siku ya Jumatano jioni na maafisa wanachunguza kupitia kamera za CCTV.

Hakuna aliyekamatwa mpaka sasa.                   

Calvin Klein ambaye ni mbunifu wa mavazi hajasema lolote kuhusiana na tukio hilo.

Chanzo: BBC
Imetafsiriwa na Mwandishi wetu

No comments:

Post a Comment