Tuesday 17 February 2015

MTOTO ALBINO AKUTWA KAKATWA MIGUU TANZANIA



Albino boys in Tanzania

Mtoto mdogo albino ambaye hakujulikana alipo tangu siku ya Jumapili amepatikana kaskazini mwa Tanzania, huku miguu yake yote miwili ikiwa imekatwa.

Watu wawili wamekamatwa wakihusishwa na kifo chake.

Awali kulikuwa na hofu kuwa huenda ameuliwa na waganga wa kienyeji wanaopiga ramli.

Polisi walisema Yohana Bahati mwenye umri wa mwaka mmoja alichukuliwa na watu waliovamia nyumba ya mama yake, na kumpiga na panga.

Viungo vya albino, husakwa na waganga wa kienyeji wanaopiga ramli nchini Tanzania.

Nchi hiyo ilipiga marufuku waganga wa kienyeji kuendeleza shughuli zao mwezi Desemba katika jaribio la kuzuia mashambulio na utekajinyara.

Baba wa mtoto huyo, aliyekuwa karibu wakati wa shambulio hilo, anahojiwa, mkuu wa polisi wa kanda hiyo Joseph Konyo aliliambia shirika la habari la AFP.




No comments:

Post a Comment