Friday 13 February 2015

MADEREVA WANAWAKE SAUDIA 'WAACHIWA HURU'



Loujain al-Hathloul at wheel of her car

Wanawake wawili kutoka Saudi Arabia waliotiwa kizuizini kwa kukiuka amri ya ufalme wa nchi hiyo kwa kuwepo madereva wanawake wameachiliwa huru baada ya zaidi ya siku 70, ripoti zinasema.

Loujain al-Hathloul, mwenye umri wa miaka 25, alikamatwa baada ya kufanya kampeni ya amri hiyo kupunguzwa makali.

Rafiki yake Maysa al-Amoudi, mwenye umri wa miaka 33, alitiwa kizuizini alipoenda kumsaidia.

Wasiwasi mkubwa uliibuka baada ya kutolewa ripoti kuwa kesi yao itahamishwa katika mahakama ya kigaidi.

Saudi Arabia ni nchi pekee kukataza wanawake kuendesha gari.

Japo si kinyume cha sheria kwa mwanamke kuendesha, ni wanaume tu wanaopewa leseni ya udereva – na wanawake wanaoendesha gari hadharani wako hatarini kupewa faini na kukamatwa na polisi.

Wanawake wa Saudi Arabia walianzisha mfululizo wa kampeni – ikiwemo kwenye mitandao ya kijamii – wakitaka sheria hiyo ilegezwe.

Bi Hathloul alikamatwa Desemba 1 baada ya kujaribu kuendesha gari ndani ya ufalme huo kutoka nchi jirani ya United Arab Emirates (UAE).

Bi al-Amoudi, mwandishi wa habari wa UAE, naye pia alikamatwa alipowasili mpakani kumwuunga mkono Bi Hathloul.

No comments:

Post a Comment