Monday 16 February 2015

WASHTAKIWA KWA MAUAJI YA COPENHAGEN



 

Polisi wa Denmark imewashutumu watu wawili kwa kuwasaidia watu wenye silaha walioua watu wawili katika mashambulio tofauti Copenhagen.

Mshukiwa huyo mwenye silaha, aliyetajwa na vyombo vya habari vya Denmark kuwa Omar El-Hussein, alipigwa risasi na polisi na kufa baada ya kushambulia mjadala wa uhuru wa kusema na sinagogi.

Mkurugenzi wa filamu na mlinzi wa sinagogi waliuawa huku watano wakijeruhiwa.

Watu hao wawili wanashtakiwa kwa kutoa na kutupa silaha, na pia kuwasaidia watu hao wenye silaha kujificha.

Wakili wa upande wa utetezi alisema watu hao wamekana mashtaka hayo.

No comments:

Post a Comment