Friday 6 February 2015

FAMILIA 'YAMUAGA' BOBBI KRISTINA BROWN



Bobbi Kristina Brown's Family Gathering at Hospital
Si  taarifa amabzo familia ya Bobbi Kristina Brown ingependa kusikia.  
 
Jumatano, siku nne baada ya binti huyo mwenye umri wa miaka 21 kukutwa hana fahamu nyumbani kwake, daktari ameiambia familia yake kuwa hakuna kinachoweza kufanyika .

 "Kila mmoja anakuja hospitali  kusema kwaheri ," alisema mmoja wa wanafamilia.  

Taarifa hizo zilimshtua hasa baba yake, Bobby Brown. "Bobby amekuwa akilia mfululizo tangu jana" kilisema chanzo hicho. "Tunaomboleza."

Mwanafamilia mwengine wa pili alikwenda hospitali usiku kuaga – na kukiri kuwa taarifa hizo za kushtua ni  ngumu sana kuamini.

"Ukimwona, utasema labda kalala tu ," kimesema chanzo hicho.

Chanzo kimoja chenye ukaribu sana na familia hiyo kimesema wamekuwa wakifanya swala karibu na kitanda chake tangu mwanzoni mwa juma  na licha ya taarifa hizo za kushtusha, “bado wana matumaini”.

Chanzo: www.people.com         
Imetafsiriwa na Mwandishi wetu        

No comments:

Post a Comment