Friday 27 February 2015

MWIMBAJI MAARUFU RWANDA AFUNGWA MIAKA 10


 Rwandan musician Kizito Mihigo in April 2014

Mwimbaji maarufu wa Rwanda amepewa kifungo cha miaka 10 gerezani baada ya kukutwa na hatia ya kuwa na mpango wa kumwuua Rais Kagame na kuchochea chuki dhidi ya serikali.

Awali Kizito Mihigo alikiri kosa na kuomba msamaha, ikimaanisha hukumu yake imepunguzwa.

Mwenzake aliyetuhumiwa naye, Cassien Ntamuhanga, mkurugenzi wa kituo cha redio cha Kikristo, amefungwa kwa miaka 25 jela kwa kosa la ugaidi na uchochezi.

Aliendelea kukana tuhuma zote.

Mihigo alikiri kuwasiliana kwa ujumbe mfupi wa simu na kundi la upinzani lenye makao makuu Afrika Kusini, la Rwanda National Congress (RNC).

Alifutiwa makosa ya ugaidi huku Ntamuhanga akifutiwa kosa la jaribio la kumwuua Rais Kagame.

Licha ya Mihigo kukiri makosa yote yanayomkabili, wakili wake baadae alisema kulikuwa hakuna ushahidi wowote wa kumtia hatiani.

Patrick Karegeya ni mmoja wa waanzilishi wa RNC, aliyekuwa mkuu wa ujasusi wa Rwanda ambaye aliwahi kuwa mshirika wa Rais Kagame.

Karegeya alikutwa amekufa nchini Afrika kusini mwaka jana huku washirika wake, familia na mamlaka za Afrika kusini zikiilaumu serikali ya Rwanda, iliyokataa kuhusika na mauaji hayo.

No comments:

Post a Comment