Friday 20 February 2015

KIMA ATARAJIWA KUACHIWA URITHI WOTE



Shabista with Chunmun

Wanandoa wa India waliotengwa baada ya familia zao kutoridhishwa na ndoa yao wameamua kuacha mali zao zote kwa kima wao.

Brajesh Srivastava na mkewe Shabista waliiambia idhaa ya Hindi ya BBC kuwa walikuwa "wapweke kwa miaka mingi" kabla ya kumnunua kima huyo aitwaye Chunmun, mwaka 2005 kwa rupia 500 yaani dola 8.

Wanandoa hao, ambao hawana watoto, wanasema wamemlea kama mtoto wao.

Bw Srivastava ni Hindu na mkewe Mwislamu, na ndoa za imani tofauti bado zina utata katika baadhi ya maeneo India.

Brajesh Srivastava and wife Shabista
Bi Srivastava alisema familia zao zote mbili ziliwatenga baada ya ndoa yao na walikuwa wapweke mpaka walipomnunua Chunmun.

"Wakati huo alikuwa mtoto, alikuwa chini ya umri wa mwezi mmoja, na mama yake alikufa kutokana na umeme," alisema.

Humnywisha Chunmun maziwa, matunda na chakula chochote anachopika. Chumba chake kina feni ambacho hutumika wakati wa joto na ‘heater’ wakati wa baridi.

No comments:

Post a Comment