Wednesday 25 February 2015

SHERIA YA UISLAM YA 1912 YABADILISHWA AUSTRIA



Protesters hold banners during the demonstration under the slogan "New Islam Law? Not with us!" in front of the parliament building in Vienna, Austria, 24 February 2015

Bunge la Austria limepitisha mabadiliko yenye utata katika sheria ya zaidi ya karne moja kuhusu Uislam.

Muswada huo, ambao nusu yake una nia ya kupambana na msimamo mkali wa Kiislam, unawapa Waislamu ulinzi wa kisheria lakini kuzuia ufadhili wa kigeni kwa ajili ya misikiti na ma-imam.

Waziri wa Uhamiaji wa Austria, Sebastian Kurz, alitetea mabadiliko hayo lakini viongozi wa Kiislamu walisema nchi hiyo inashindwa kuwapa haki sawa.

Sheria ya mwaka 1912 iliifanya Uislamu kuwa dini rasmi Austria.

Imeheshimiwa sheria hiyo kwa muda mrefu kuwa mfano wa kusimamia Uislam barani Ulaya.

Utaratibu mpya, uliyopendekezwa kwa mara ya kwanza miaka mitatu iliyopita, unaheshimu sikukuu za kidini na mafunzo kwa ma-imam.

Lakini makundi ya Kiislam yalisema kuzuia ufadhili kutoka nchi za nje si haki kwani misaada ya imani za Kikristo na Kiyahudi bado inaruhusiwa.

Walisema sheria hiyo inaonyesha kutokuwa na imani kwa kiwango kikubwa na Waislam huku baadhi wakipanga kuipinga kwenye mahakama ya katiba.

Bw Kurz aliiambia BBC "Tunachotaka ni kupunguza ushawishi wa kisiasa na udhibiti wa nje na tunataka kuupa Uislam nafasi ya kuimarika kwa uhuru zaidi ndani ya jumuiya yetu ikiambatana na taratibu zetu za Ulaya.”

No comments:

Post a Comment