Wednesday 25 February 2015

DRC YAANZA MAPAMBANO NA WAASI WA KIHUTU



Democratic Republic of Congo regular army soldiers stand guard in the Nakabumbi area of Kimbumba, 20kms from Goma, near the border with Rwanda, on June 14, 201

Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo imeanza mashambulio dhidi ya waasi wa Kihutu wa Rwanda mashariki mwa nchi hiyo.

Awali mawaziri waliahidi kupambana na wapiganaji wa FDLR baada ya kushindwa kufika makataa ya kusalimisha silaha zao mwezi uliopita.

Waasi wa Kihutu walihusika katika mauaji ya kimbari nchini Rwanda mwaka 1994.

Majeshi ya kutunza amani ya Umoja wa Mataifa DRC ilijitoa kuunga mkono harakati hizo kwasababu ya majenerali wawili wa serikali wanatuhumiwa kukiuka haki za binadamu.

Mashambulio hayo ya Jumanne yalifanyika mashariki mwa Congo katika jimbo la Kivu ya Kaskazini, takriban kilomita 10 kutoka kwenye mpaka na Burundi, jeshi hilo lilisema.

No comments:

Post a Comment