![]() |
Ivory Coast wameshinda taji la Kombe la Afrika mwaka 2015 kwa mikwaju 9 ya penati Ghana 8 |
Timu ya soka ya Ivory Coast imenyakuwa taji la Kombe la Afrika la mwaka 2015 kwa kuitandika timu ya Ghana kwa mikwaju ya penati.
Ivory Coast imeshinda kwa mikwaju 9 ya penati huku Ghana ikipata mikwaju 8.
Boubacar Barry, 35, ndiye aliyeibuka kidedea kwa kufunga penati ya mwisho baada ya mlinda mlango wa Ghana Razak Braimah kukosa penati.
![]() |
Ghana walipata penati nane huku Ivory Coast wakishinda kwa penati tisa |
Mlinda mlango mkongwe wa Ivory Boubacar Barry ndiye nyota wa mchezo wa leo.
Mashindano hayo yalikuwa yanafanyika nchini Equatorial Guinea.
Chanzo: taarifa.co.tz
No comments:
Post a Comment