Monday 9 February 2015

IVORY COAST YASHINDA KOMBE LA AFRIKA 2015

Ivory Coast wameshinda taji la Kombe la Afrika mwaka 2015
Ivory Coast wameshinda taji la Kombe la Afrika mwaka 2015 kwa mikwaju 9 ya penati Ghana 8

Timu ya soka ya Ivory Coast imenyakuwa taji la Kombe la Afrika la mwaka 2015 kwa kuitandika timu ya Ghana kwa mikwaju ya penati.

Ivory Coast imeshinda kwa mikwaju 9 ya penati huku Ghana ikipata mikwaju 8.

Boubacar Barry, 35, ndiye aliyeibuka kidedea kwa kufunga penati ya mwisho baada ya mlinda mlango wa Ghana Razak Braimah kukosa penati.

Ghana walipata penati 8 huku Ivory Coast wakishinda kwa penati 9
Ghana walipata penati nane huku Ivory Coast wakishinda kwa penati tisa

Mlinda mlango mkongwe wa Ivory Boubacar Barry ndiye nyota wa mchezo wa leo.

Mashindano hayo yalikuwa yanafanyika nchini Equatorial Guinea.


Chanzo: taarifa.co.tz

No comments:

Post a Comment