Wednesday 25 February 2015

JAMAICA SASA KUHALALISHA BANGI



 Jah P., left, and Jah Henry, smoke marijuana from a chillum pipe in Kingston, Jamaica, Wednesday, Aug. 18, 1999.

Jamaica imefuta suala la kumiliki kiwango kidogo cha bangi kuwa ni uhalifu kwa matumizi binafsi.

Bunge la nchi hiyo limepitisha sheria iliyokuwa na mjadala mzito kuruhusu kumiliki hadi gramu 57 za ‘marijuana’.

Pia itaruhusu mamlaka husika kutathmini matumizi ya kitabibu na kisayansi wa mmea huo.

Marijuana inalimwa kwa kiwango cha juu Jamaica na ina mizizi ya kiutamaduni.

Kisiwa hicho kinadhaniwa kuwa kikubwa kwa visiwa vya Carribean kuuza marijuana nje – ambapo hujulikana pia kwa jina la ganja na cannabis Marekani.

Uamuzi wake wa kulegeza masharti ya matumizi ya bangi ndani ya taifa hilo kunaashiria kama makubaliano fulani ya kidunia.

Nchi tele za Latin America na Marekani – na hivi karibuni Alaska – wamehalalaisha matumizi ya bangi hizo katika miaka ya hivi karibuni.

No comments:

Post a Comment