Tuesday 3 February 2015

RUBANI WA JORDAN 'ACHOMWA AKIWA HAI'





Jordan imethibitisha kifo cha rubani Moaz al-Kasasbeh baada ya video iliyowekwa mtandaoni na Islamic State (IS) inayodaiwa kumwonyesha akichomwa moto akiwa hai.

Video hiyo inamwonyesha mtu mmoja akiwa amesimama kwenye kizimba huku akiwaka moto.

Maafisa wanahangaika kuthibitisha kama video hiyo ni ya kweli.

Mfalme Abdullah wa Jordan amemsifu Lt Kasasbeh kuwa shujaa, akisema Jordan lazima “isimame imara” wakati huu mgumu.

Rubani huyo alikamatwa baada ya ndege yake kushuka karibu na Raqqa, Syria, mwezi Desemba wakati wa harakati za mapambano dhidi ya IS.

Video iliyowekwa siku ya Jumanne ilisambazwa kwenye mtandao wa kijamii wa Twitter inayojulikana kuwa chanzo cha propaganda za IS.

No comments:

Post a Comment