Thursday 30 October 2014

GRACA ATAKA MWANAMKE KUMRITHI MUSEVENI




Uganda inatakiwa kuwa na rais mwanamke baada ya Rais Yoweri Museveni kustaafu, mke wa aliyekuwa rais wa Afrika kusini alisema.

 Mwanaharakati wa haki za wanawake na watoto, Graca Machel, alisema Uganda ni miongoni mwa nchi za Afrika zenye wanawake hodari ambao wana uwezo wa kuwa rais. 

“Sijui rais Museveni ana mpango wa kustaafu lini, mwaka 2016? Sijui, lakini atakapofanya hivyo, mwanamke lazima ajiandae kuwa Rais. Ntamwambia (Museveni) tutakapokutana,”  aliyasema hayo huku akishangiliwa katika hoteli ya Serena mjini Kampala.

Machel alisikitika alipoarifiwa kuwa Dr. Specioza Wandira Kazibwe hakuwa makamu wa rais tena kwa sasa.

Rais Museveni aliweka historia alipomteua Dr. Kazibwe kuwa makamu wa rais wa kwanza Uganda mwaka 1994.

Alishikilia nafasi hiyo hadi mwaka 2003. Machel ni mjane wa aliyekuwa rais wa Afrika kusini Nelson Mandela.

Chanzo: newvision.co.ug
Imetafsiriwa na Mwandishi wetu
                                   



No comments:

Post a Comment