Thursday 30 October 2014

BW GOODLUCK AGOMBEA TENA URAIS NIGERIA



Nigerian President Goodluck Jonathan at the World Economic Forum on Africa in Abuja (10 October 2014)

Rais wa Nigeria Goodluck Jonathan amethibitisha kugombea tena urais katika uchaguzi unaotarajiwa kufanyika mwezi Februari, ofisi yake imesema.

Mpaka sasa alikuwa akikataa kuthibitisha nia yake ya kuchuana tena kwenye kinyang’anyiro hicho.

Nia yake hiyo inatangazwa huku akiwa anakosolewa vikali siku hadi siku kutokana na namna anavyoshughulikia suala la wapiganaji wa Boko Haram waliowateka zaidi ya mabinti 200.

Wapiganaji wameripotiwa kudhibiti mji wa Mubi kaskazini-mashariki mwa nchi hiyo.

Serikali ilitangaza kusimamisha mapigano na Boko Haram mapema mwezi huu ambapo ingetakiwa mabinti hao wanafunzi waachiwe huru.

Maelfu ya watu wamekimbia ngome ya waasi hao iliyopo kaskazini-mashariki wakati wote wa mgogoro huo.

No comments:

Post a Comment