Monday 27 October 2014

MLINDA MLANGO WA AFRIKA KUSINI AUAWA






Msako mkali unafanyika kutafua wauaji wa  Kapteni wa soka wa Afrika kusini Senzo Meyiwa, polisi wamesema.

Wametangaza kutoa zawadi ya rand 250,000  (£14,100; $22,800) kwa taarifa zozote zitakazosaidia kukamatwa kwa wanaoshutumiwa kuwa wezi waliompiga risasi na kumwuua.

Imeripotiwa alishambuliwa baada ya wanaume wawili kuingia kwenye nyumba ya mpenzi wake huko Vosloorus, kusini mwa Johannesburg.

Watu hao waliingia na kutaka watoe simu zao za mkononi na mali nyingine. Mwanamme mwengine wa tatu alibaki nje.

Mmoja miongoni mwa wawili hao ameelezewa na polisi kuwa mrefu, mweusi, mwembamba na mwenye rasta, na mwengine ni mfupi, mweusi na mkuza.

Rais Jacob Zuma alitoa salaam za rambirambi kwa mlinda mlango huyo, akisema, “hakuna maneno yanayoweza kuelezea mshtuko taifa limepata kutokana na kifo hicho”.

Wakala wake amemwelezea kuwa mtu asiyekuwa na makuu, aliyetoka katika maisha magumu na kufanikiwa kuwa “shujaa katika jicho la kila mmoja”.

Kijana huyo mwenye umri wa miaka 27 alikuwa mlinda mlango wa Orlando Pirates na aliichezea Afrika kusini katika mashindano manne ya mwisho ya mechi za kufuzu kombe la Mataifa Afrika.

Siku ya Jumamosi, alikuwa na klabu yake, walipovuka nusu fainali ya kombe la Ligi la Afrika kusini, baada ya kuinyuka Ajax Cape mabao 4 -1.


No comments:

Post a Comment