Sunday 26 October 2014

CHAMA TAWALA BOTSWANA KUSHINDA UCHAGUZI



 Polling officers count ballot boxes at a counting centre in Gaborone on 24 October 2014 during the Botswana general elections.

Chama tawala cha Botswana Democratic (BDP) kimeshinda uchaguzi mkuu katika nchi inayozalisha almasi kwa wingi zaidi duniani.

Imepata takriban viti 33 miongoni mwa 57 vya ubunge, tume ya uchaguzi ya taifa imesema.

Chama kinahitaji viti 29 kuchukua madaraka. Kundi la upinzani la Umbrella for Democratic Change limepata viti 14.

Chama cha BDP cha Rais Ian Khama kimekuwa madarakani tangu Botswana ilipopata uhuru mwaka 1966.

Lakini kimekuwa kikipambana kuungwa mkono maeneo ya mijini ambapo vyama vya upinzani hivi karibuni vimeonekana kufanya vizuri.

Botswana inaonekana ni miongoni mwa nchi zenye utulivu na demokrasia barani Afrika.

Nchi hiyo bado haina mgawanyiko sawa wa mali, umaskini wa hali ya juu, ukosefu wa ajira na HIV, kulingana na Benki ya Maendeleo ya Afrika ADB.

Ukosefu wa kiwango cha ajira umefikia 17.8% na ina watu wenye maambukizi ya virusi vya HIV kwa 23.4%.

Utafiti uliofanyika mwezi huu na shirika la utafiti la Afrobarometer limeripoti 58% ya watu wa Botswana wanaona ukosefu wa ajira kama tatizo kubwa linaloikumba nchi yao ya Botswana.

No comments:

Post a Comment