Sunday 26 October 2014

MKIMBIAJI WA AFRIKA KUSINI AFARIKI DUNIA



 

Aliyekuwa mshindi wa dunia wa mbio za mita 800 Mbulaeni Mulaudzi amefariki dunia katika ajali ya gari nchini mwake Afrika kusini.

Mulaudzi alishinda dhahabu katika mashindano ya dunia ya mwaka 2009 katika mita 800 mjini Berlin na kushinda fedha katika mashindano ya Olimpiki mwaka 2004 mjini Athens.

Kijana huyo mwenye umri wa miaka 34, aliyebeba bendera ya nchi yake katika sherehe za ufunguzi mjini Athens, alistaafu mwaka 2013.

"Bw Mulaudzi kwa hakika alikuwa miongoni mwa wakimbiaji bora Afrika kusini iliyowahi kushuhudia,” alisema Peet van Zyl 
Chanzo: BBC
Imetafsiriwa na Mwandishi wetu


No comments:

Post a Comment