Thursday 23 October 2014

WAKASIRISHWA KUZUIWA KUBUSU, ZIMBABWE



The University of Zimbabwe circular
Orodha ya vitu 11 vya utovu wa nidhamu
Kukatazwa kubusiana kwa wanafunzi iliyotolewa na chuo kikuu cha Zimbabwe ‘haina maana’, mwakilishi wa wanafunzi aliiambia BBC.

Vipeperushi kutoka mamlaka za chuo zimesema wale “watakaokutwa kwenye hali zenye utata” kwenye chuo hicho kilichopo mjini Harare watachukuliwa hatua.

“Kwa umri huu kuambiwa huruhusiwi kubusu au kumkumbatia mtu...si sawa. Tsitsi Mazikana alisema.

Chuo hicho hakijasema chochote hadi sasa kuhusu uamuzi huo wa wanafunzi kupinga suala hilo.

Mwanzo wa mwaka wa masomo kulitolewa kama sehemu ya orodha ya “ utovu wa nidhamu unaosababisha mtu kufukuzwa kwenye makazi ya chuo”.

Miongoni mwa masharti 11 pia inakatazwa kula vyumbani.

No comments:

Post a Comment