Sunday 26 October 2014

HUKUMU YA KIFO YA BI JABBARI YATEKELEZWA



A picture taken on December 15, 2008 at a court in Tehran shows Iranian Reyhaneh Jabbari speaking to defend herself during the first hearing of her trial for the murder of a former intelligence official.
Bi Jabbari alitengwa kwa miezi miwili baada ya kukamatwa na kesi yake kuanza mwaka 2008

Iran imeendelea na kutekeleza hukumu ya kifo kwa mwanamke mmoja licha ya kampeni ya kimataifa ya kusihi hatua hiyo isitishwe.

Reyhaneh Jabbari, mwenye umri wa miaka 26, aliuliwa kwa kunyongwa kwenye gereza la Tehran siku ya Jumamosi asubuhi.

Alitiwa hatiani kwa kumwuua mwanamme mmoja ambaye alisema alikuwa akijaribu kumdhalilisha kijinsia.

Jabbari alikamtwa mwaka 2007 kwa mauaji ya Morteza Abdolali Sarbandi, aliyekuwa mfanyakazi wa wizara ya masuala ya kijasusi.

Mama yake Bi Jabbari's, Shole Pakravan, aliiambia BBC alimtembelea binti yake muda kidogo kabla ya hukumu hiyo kutekelezwa.

Wizara ya mambo ya nje ya Marekani na Uingereza zote zimelaani mauaji hayo.

"Umoja wa Mataifa umesema kutiwa kwake hatiani kulitokana na madai aliyoyatoa baada ya kupewa vitisho. Ninasihi Iran kuahirisha hukumu zote za kifo," alisema waziri wa mambo ya nje wa Uingereza.

Kampeni ya kutoa wito wa kusitisha mauaji hayo yalianzishwa katika mitandao ya kijamii ya Facebook na Twitter mwezi uliopita na ilionekana iliweza kusimamisha kifo hicho kwa muda tu.

Hatahivyo, shirika la habari la serikali Tasnim lilisema Jumamosi kuwa hukumu hiyo ya kifo kwa Jabbari ilitekelezwa baada ya ndugu zake kushindwa kupata msamaha kutoka kwa familia ya Morteza.

Lilisema madai yake ya kumwuua kwa minajil ya kujilinda haikuweza kuthibitishwa mahakamani.

Ukurasa wa Facebook ulioanzishwa sasa unasema “Mungu amlaze pahala pema”.

No comments:

Post a Comment