Monday 27 October 2014

QATAR YAKANA KUWAFADHILI IS



 Islamic State militant waves flag in Raqqa, Iraq, on 29 June 2014

Maafisa waandamizi kutoka Qatar wamekana vikali madai kuwa nchi hiyo inaunga mkono makundi ya kigaidi nchini Syria kama vile kundi linalojiita Islamic State IS.

Wameiambia BBC kwamba Qatar ilitoa misaada kwa wapiganaji wa wastani tu, wakishirikiana na shirika la kijasusi la Marekani CIA, na mashirikia mengine ya kijasusi ya Kiarabu na nchi za magharibi.

Udhibiti mkali wa fedha nao umewekwa, waliongeza.

Kauli hizo zimetolewa kabla ya ziara ya kiongozi wa Qatar Sheikh Tamim bin Hamad Al Thani nchini Uingereza wiki hii.

Mapema mwezi huu iliripotiwa kuwa wabunge kadhaa walihoji ukaribu wa Uingereza na Qatar, huku kukiwa na madai kuwa wana uhusiano na kundi la IS.

Mwandishi wa ulinzi wa BBC alisema Qatar, mwekezaji mkuu wa Uingereza, ameshtushwa sana na madai hayo.

No comments:

Post a Comment