Friday 24 October 2014

WANAWAKE 'WAGOMA' KUFANYA MAPENZI, SUDAN K



Displaced South Sudanese women carry their possessions
Kuna zaidi ya wakimbizi wa ndani milioni 1.4 Sudan kusini

Wanaharakati wa kuleta amani wanawake Sudan Kusini wamependekeza kuwe na mgomo wa kitaifa wa kutofanya mapenzi ili kusimamisha mapigano ya wenyewe kwa wenyewe nchini humo.

Wanaharakati hao wanataka wanawake wawaunge mkono kwa matumaini ya kuwa itawashawishi wanaume kutafuta suluhu ya amani kutokana na mgogoro uliopo.

Gazeti la Sudan Tribune limeripoti kuwa wazo hilo lilitolewa katika mkutano wa zaidi ya wanaharakati wa kike 90, wakiwemo wabunge, katika mji mkuu wa Sudan kusini, Juba.

Waandalizi wa mkutano huo walisema, “Pendekezo kuu ni kuwashawishi wanawake wa Sudan kusini kuwanyima haki ya kufanya mapenzi waume zao mpaka amani irejee nchini”.

Serikali ya Sudan kusini imekuwa ikipigana na waasi tangu Desemba 2013.

Maelfu ya watu wamekimbilia nchi jirani, na watu milioni 1.4 ni wakimbizi wa ndani kutokana na mgogoro huo, kulingana na Umoja wa Mataifa.

Chanzo: BBC
Imetafsiriwa na Mwandishi wetu

No comments:

Post a Comment