Wednesday 10 September 2014

FAIDA YA MAN UNITED 'KUTETEREKA'


Aliyekuwa meneja wa Man United, David Moyes


Manchester United imetangaza kuporomoka kwa faida ya kila mwaka wa fedha katika mwaka ambao David Moyes alikuwa meneja. 

Klabu hiyo ya Ligi Kuu ya England imesema kipato halisi kimeporomoka kwa asilimia 84 na kufikia takriban dola milioni 45. 

Klabu hiyo imesema inatarajia mapato yake ya mwaka 2015 kushuka kutokana na klabu hiyo kushindwa kufuzu kucheza Klabu Bingwa Ulaya kwa mara ya kwanza tangu msimu wa mwaka 1994-95. 

Klabu hiyo imesema Moyes na wasaidizi wake walilipwa zaidi ya dola milioni 8 kama fidia kufuatia kufukuzwa kazi mwezi Aprili, chini ya mwaka mmoja tangu apewe kazi hiyo.

Chanzo: FB - Salim Kikeke

No comments:

Post a Comment