Monday 15 September 2014

MALAYSIA YAWATUMIA GLOVU AFRIKA MAGHARIBI

 A medical worker in Kailahun, Sierra Leone washes their gloves in chlorine on 15 August 2014.
Malaysia ina mpango wa kutoa zaidi ya glovu za mpira milioni 20 za kujukinga katika nchi tano barani Afrika zilioathirika na mlipuko wa Ebola, serikali ya nchi hiyo imesema

Zitasambazwa kwa wahudumu wa afya nchini Liberia, Sierra Leone , Guinea, Nigeria na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.

Upungufu wa vifaa vya kujikinga imekuwa sababu moja ya kusambaa kwa virusi hivyo.

Maradhi  hayo yameua zaidi ya watu 2,400, wengi wao wakiwemo wahudumu wa afya, mwaka huu, katika mlipuko mbaya kutokea duniani.

Wahudumu wa afya hivi karibuni waligoma nchini Liberia, wakisema wanahitaji vifaa zaidi vya kujikinga.

Malaysia inaongoza kwa uzalishaji wa glovu za mpira, ikitengeneza 60% ya glovu hizo duniani.

Chanzo: BBC
Imetafsiriwa na Mwandishi wetu

No comments:

Post a Comment