Friday 12 September 2014

WASHUKIWA WALIOMPIGA RISASI MALALA MBARONI

Pakistani schoolgirl activist Malala Yousafzai poses for pictures during a photo opportunity at the United Nations in the Manhattan borough of New York on 18 August 2014.
Malala alikuwa na umri wa miaka 15 tu alipopigwa risasi mara tatu kichwani
Wapiganaji wanaoshukiwa kumpiga risasi mwanaharakati Malala Yousafzai wamekamatwa, jeshi la Pakistan limesema.

Binti huyo alipigwa risasi kichwani na wapiganaji wa Kitaleban mwezi Oktoba 2012 kutokana na kampeni yake kuhusu elimu kwa watoto wa kike.

Walipanda kwenye basi lake la shule kaskazini-magharibi mwa Pakistan na kufyatua risasi, katika shambulio ambalo liliwajeruhi pia marafiki zake wawili.

Tangu wakati huo anaendelea vizuri kutokana na shambulio hilo, lililoishtua dunia na kumpa umaarufu ulimwenguni kote.

Alitajwa kama mmoja wenye ushawishi mkubwa duniani na jarida la Time mwaka 2013, aliteuliwa kupata tuzo ya Amani ya Nobel na amezindua hivi karibuni kitabu cha maisha yake.

Msemaji wa jeshi Jenerali Asim Bajwa alisema wanachama 10 wa kundi la TTP wamekamatwa katika harakati za pamoja za kijeshi na Pakistan, polisi na majasusi.

Jenerali Bajwa aliongeza kuwa, kundi hilo limekuwa likifanya kazi chini ya maelekezo ya Mullah Fazlullah,mkuu wa Taliban ya Pakistan.

Malala Yousafzai, aliyekuwa na umri wa miaka 15 wakati wa shambulio hilo, tayari alipata umaarufu kwa kudai haki za elimu na watoto nchini Pakistan.

Chanzo: BBC
Imetafsiriwa na Mwandishi wetu


No comments:

Post a Comment