Thursday 11 September 2014

PISTORIUS AFUTIWA MASHTAKA YA MAUAJI


Jaji katika kesi ya Oscar Pistorius imemfutia mashtaka ya mauaji, lakini ameacha kutoa hukumu ya kosa la kuua bila kukusudia (culpable homicide) kwa mwanariadha huyo mpaka siku ya Ijumaa

Jaji Thokozile Masipa alisema waendesha mashtaka hawakutoa ushahidi wa kutosha kuonyesha kuwa alidhamiria kumwuua mpenzi wake Reeva Steenkamp, na kusababisha machozi kumtoka mkimbiaji huyo wa Olimpiki wa mbio fupi.

Lakini alisema alifanya uzembe. Bw Pistorius alisema alidhani kulikuwa na mtu asiyemfahamu  chooni kwake.

Kabla ya kuahirisha kesi hiyo, jaji huyo alisema mtu makini asingefyatua risasi

Mwandishi wa BBC Andrew Harding , aliyekuwa mahakamani mjini Pretoria, alisema jaji huyo anatarajiwa kutoa uamuzi wa kuua bila kukusudia.

Awali, Jaji Masipa alimwelezea Bw Pistorius kama shahidi anayekwepa lakini haimaanishi kuwa ana hatia.

Akimfutia mashatka ya mauaji, alisema asingeona mtu anayemwuua nyuma ya mlango wa chooni.

Mkimbiaji huyo wa Afrika kusini alikana kumwuua Bi Steenkamp baada ya mfarakano siku ya Valentine mwaka jana, akisema amempiga risasi kwa bahati mbaya.

Bw Pistorius, mwenye umri wa miaka 27, amekana mashtaka yote yanayomkabili, ikiwemo kufaytua risasi hadharani na kumiliki risasi kinyume cha sheria.


No comments:

Post a Comment