Tuesday 9 September 2014

DENZEL AKUMBUKA MACHUNGU YA KUBAGULIWA



Muigizaji maarufu Denzel Washington na mkewe Pauletta Washington


 Wakati wa kutayarisha filamu mpya iitwayo The Equalizer mjini Boston, Marekani, Denzel Washington aliibua kumbukumbu za ubaguzi alizokabiliana nazo zaidi ya miaka 30 iliyopita.

Washington alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari katika tamasha la Filamu la Toronto, ndipo lilipoibuka swali kuhusu kuigiza filamu hiyo Boston na kauli aliyoitoa kuhusu mke wake ndiyo iliyoleta hisia zisizotarajiwa.

Washington alieleza wakati alipokuwa Boston miongo mitatu iliyopita pamoja na mkewe Pauletta Learson Washington, aliyekuwa naye akiigiza, baadhi ya watu wakadhani yeye ni kuwadi, na mkewe ni changudoa. Walinzi waliitwa, na ghasia zikaanza.

“Nilikuwa sijui kupigana, lakini nilijua namna ya kushinda,” Washington aliwaambia waandishi wa habari.

Pia anakumbuka namna alivyokwenda kumtazama mkewe akiigiza usiku mmoja na kuitwa kwa jina la N (ambalo halifai kulitaja)

 “‘Hey n—, n—, n—, n—, hey boy.’ Nikasema Nini?.’  Hiyo ndio kumbukumbu niliyonayo ya Boston ,” alisema.

Halafu akaelezea mara ya kwanza alipoitwa kwa jina hilo linaloanzia N alipokuwa Florida, alikuwa amekaa kwenye veranda akiwa kama na umri wa miaka tisa. Aliitwa jina hilo lenye dharau na kundi la watoto ambapo alirudi nyumbani na kumwuuliza mama yake kwanini wanamwita hivyo.

 “Akasema, Ah, huyo ni mtu tu anaogopa utachukua nafasi yake.’ Ilikuwa kama kaa chini ya mtungi. Na kusinimagharibi mwa Boston, ilikuwa kawaida ,” alisema, akimaanisha nyumba kwenye maeneo yenye umaskini ambazo zimebanana. “Wao wako chini. Kwahiyo ilikuwa kama kusema, ‘Sisi bora kuliko wewe.’ Ndio, kwahiyo nimekuja Boston na kumbukumbu kama hizo.”

The Equalizer itaanza kuonyeshwa Marekani Sepembat 26.

Chanzo: uk/yahoo.com
Imetafsiriwa na Mwandishi wetu


No comments:

Post a Comment