Thursday 18 September 2014

MTANZANIA AKABILIWA MIAKA 20 JELA, MAREKANI





Alikuwa akiishi maisha ya kipekee kwenye ardhi yenye ufahari na makuu tele, ambayo wengi nyumbani Tanzania wasingewaza kutokea. Amon Rweyemamu Mtaza alionekana kuishi maisha ya juu sana nchini Marekani, ilivyokuwa ikionekana.

Alikuwa na tatizo moja tu: Utajiri wake ulijengwa kwenye misingi ya uongo – kuwalaghai wanaopokea malipo ya uzeeni yaani pensheni. Na sasa hali halisi imemrudia Mtaza mwenye umri wa miaka 38.

Raia huyo wa Tanzania anayeishi Huoston, Texas, anakabiliwa na kifungo cha miaka 20 jela kwa kufanya udanganyifu katika masuala ya kodi akiwa na mshirika.

Imeripotiwa waliwaibia zaidi ya wazee 600 waliokuwa wakilipwa mafao ya uzeeni ambapo walipata zaidi ya dola milioni 1.8 (zaidi ya shilingi bilioni 3)

Shirika la Habari la AP liliripoti kuwa Mtaza alikiri kushiriki katika jaribio la kufanya udanganyifu kupitia mtandao na makosa mawili mazito ya wizi wa utambulisho.

Waendesha mashtaka Houston walisema Mtanzania huyo na mshirika wake ambaye ni mwanamke walihusika katika wizi huo na kuiba utambulisho wa wazee hao waliokuwa walipwe pesa za uzeeni.

Mtanzania huyo alikamatwa Machi 3.

Chanzo: The Citizen, Tanzania
Imetafsiriwa na Mwandishi wetu

No comments:

Post a Comment