Thursday 11 September 2014

UAMUZI WA OSCAR PISTORIUS WAANZA KUTOLEWA



 
Jaji kwenye kesi ya Oscar Pistorius ameanza kutoa uamuzi wake dhidi ya mwanariadha huyo, mchakato unaoweza kuchukua saa tele.

Mwanariadha huyo anakabiliwa na miaka 25 gerezani iwapo atakutwa na hatia ya mauaji ya kupanga.

Anakana kumwuua mpenzi wake kwa makusudi Reeva Steenkamp siku ya Valentine mwaka jana, akisema alidhani kulikuwa na mtu asiyemfahamu kaingia nyumbani kwake.

Jaji huyo anaweza akamhukumu kwa kosa la kuua bila kukusudia, ambapo atapata kifungo cha muda mrefu jela. .

Bw Pistorius, mwenye umri wa miaka 27, amekana kwa makosa yote yanayomkabili, ikiwemo makosa mawili ya kufyatua risasi hadharani na kumiliki silaha kinyume cha sheria.

Jaji Thokosile Masipa alianza kwa kuelezea makosa yanayomkabili mwanariadha huyo na kurudia ushahidi alioutoa, akisoma taratibu na kwa umakini.

Baada ya hapo alianza kusoma kwa ufupi kuhusu kesi hiyo.


Chanzo: BBC

                                                                                            

No comments:

Post a Comment