Saturday 13 September 2014

WANAOWAHUDUMIA WAGONJWA WA EBOLA WAGOMA




Wafanyakazi wa hospitali wameanza mgomo kwenye wodi ya Ebola ilojazana katika hospitali kuu ya wilaya mashariki mwa Sierra Leone palipoathirika zaidi na ugonjwa huo kwa madai kuwa serikali inashindwa kuwalipa.

Hadi wafanyakazi 80 walijazana kwenye mlango wa kuingilia wa hospitali hiyo siku ya Ijumaa, na kusabababisha shughuli zote kusimama.

Wafanyakazi hao walifanya mgomo kwa amani lakini walikuwa tafrani.

Tukio hilo limetokea baada ya migomo mengine kufanyika kwenye hospitali hiyohiyo kwa madai ya mazingira mabovu ya kufanyia kazi, maambukizi miongoni mwao na malipo wanayopewa haiendani na hatari wanayokabiliana nayo.

Wafanyakazi hao waliajiriwa kitaifa kuongeza idadi yao katika hospitali ya serikali ya Kenema, ambapo wanafanyia kazi kwenye hema ‘maalum lililotengwa’ wakati wauguzi na wafanyakazi wengine wakiwa na kazi ya kutibu wagonjwa, kusafisha vyombo vilivyochafuka, kusafisha vinyesi, matapishi, damu na kuondosha pamoja na kuzika maiti.

"Nilianza kufanya kazi hapa mwezi mmoja uliopita na hatujalipwa kitu wiki ya pili sasa," Umaru, anayeshughulika na usafi, aliiambia Al Jazeera. "Tumemwambia kila mmoja agome mpaka tulipwe marupurupu yetu."

Vifo vya wafanyakazi                              

Wafanyakazi waliobaki walisema zaidi ya wauguzi 38 na madaktari wameambukizwa na kufariki dunia katika eneo hilo tangu mlipuko wa ugonjwa huo kutokea, miongoni mwao ni daktari maarufu Sheik Umar Khan.

Wafanyakazi wanaosaidia kuhudumia wagonjwa wa Ebola wanatakiwa kulipwa dola 110 kwa wiki lakini wamekuwa wakifanya kazi bure huko Kenema katika kipindi cha wiki mbili zilizopita.

Eneo hilo maalum la kuhudumia wagonjwa wa Ebola limezidiwa likiwa na takriban wagonjwa 80 wakitibiwa na wapya wakiwasili kila siku.


No comments:

Post a Comment