Friday 19 September 2014

WAZIRI MKUU UGANDA AFUKUZWA NA RAIS MUSEVENI

Aliyekuwa Waziri Mkuu wa Uganda Amama Mbabazi

Rais wa Uganda Yoweri Museveni amemfukuza kazi waziri wake mkuu Amama Mbabazi.

Nafasi yake sasa inachukuliwa na Ruhakana Rugunda, ambaye kabla ya kuteuliwa alikuwa waziri wa afya.

Bw. Mbabazi amekuwa mshirika wa karibu wa Rais Museveni lakini wachambuzi wanasema ushirikiano wao umekuwa ukizorota.

Mapema mwaka huu chama tawala nchini humo kilimpitisha Rais Museveni kuwa mgombea pekee wa Urais mwaka 2016 lakini inaelezwa kuwa Bw Mbabazi alipinga uamuzi huo.

No comments:

Post a Comment