Friday 19 September 2014

USKOCHI YASEMA 'HAPANA' KWA UHURU



No supporters celebrate

Uskochi imepiga kura kubaki kwenye muungano na Uingereza baada ya wapiga kura kukataa uhuru.

Matokeo yakiwa yametoka kwenye manispaa zote 32, kura ya “Hapana” imepata 2,001,926, dhidi ya 1,617,989 waliopiga "Ndio".

Waziri kiongozi wa Uskochi ametoa wito wa kuleta umoja na vyama vya muungano kutoa madaraka zaidi.  

Waziri mkuu wa Uingereza David Cameron alisema alifurahi sana kuwa Uingereza itabaki ikiwa imeungana na ahadi za kutoa madaraka zaidi zitaheshimiwa.

Bw Cameron amesema vyama vikuu vitatu vya muungano Westminister sasa vitatekeleza ahadi ya kutoa madaraka zaidi kwa bunge la Uskochi.

"Tutahakikisha ahadi zilizotolewa zitaheshimiwa," alisema.

Alitangaza kuwa Lord Smith, ambaye aliongoza michezo ya Jumuiya za Madola huko Glasgow, atasimamia mchakatao mzima wa kutekeleza ahadi hizo, ikiwemo madaraka mapya juu ya kodi pamoja na matumizi kufikia makubaliano ifikapo mwezi Novemba, na rasimu ya bunge kuchapishwa ifikapo mwezi Januari.

Waziri mkuu naye alisema kuwa watu wa England, Wales na Ireland kaskazini lazima wawe na usemi zaidi kwenye masuala yao wenyewe.

"Huko Wales kuna mapendekezo ya kuipa serikali na bunge la Wales madaraka zaidi na ninataka Wales iwe kiini cha mjadala wa namna Uingereza itaweza kuwajibika kwa mataifa yetu yote ," alisema.


No comments:

Post a Comment