Saturday 20 September 2014

MUASI WA KIKE WA LIBERIA AKAMATWA

A photo dated 29 May 1990 shows rebel leader Charles Taylor
Charles Taylor alituhumiwa kwa kufanya ukatili wa hali ya juu

Makundi ya kutetea haki za binadamu yamefurahishwa na kukamatwa kwa kamanda wa kike wa muasi Charles Taylor nchini Belgium kwa uhalifu wa kivita unaodaiwa kufanyika wakati wa vita vya wenyewe kwa wenyewe Liberia.

Kukamatwa huko kumefanyika baada ya malalamiko kuwasilishwa kwa niaba ya watu watatu walioathrika kwenye mapigano mwaka 1992 iliyojulikana kama Operation Octopus.

Martina Johnson bado hajasema chochote juu ya madai ya kuhusika na "ukataji viungo na mauaji ya watu wengi".

Bw Taylor amefungwa kwa makosa ya uhalifu wa kivita yaliyofanyika nchi jirani ya Sierra Leone.

Mahakama maalum iliyoungwa mkono na Umoja wa Mataifa ilimkuta na hatia mwaka 2012 kwa usambazaji wa silaha kwa waasi wa Sierra Leone na badala yake kupewa kile kilichoitwa almasi haramu 'blood diamond'.

Alianzisha uasi nchini Liberia mwaka 1989, na kuwa Rais mwaka 1997- lakini alilazimika kukimbilia uhamishoni baada ya mapigano na kundi jengine la uasi mwaka 2003.


No comments:

Post a Comment