Tuesday 9 September 2014

ISRAEL 'YAWATISHIA' WAHAMIAJI KUONDOKA



African migrants stand inside the Holot facility in Israel's Negev desert (17 February 2014)

Mamia ya wahamiaji WaEritrea na WaSudan wapo kwenye eneo maalum la jangwa la Negev, Israel




Israel inatumia nguvu na vitisho kinyume na sheria kwa takriban raia 7,000 kutoka Eritrea na Sudan kuondoka nchini, shirika la kutetea haki za binadamu la Human Rights Watch limesema.

Wamenyimwa haki ya kupewa fursa ya kufuata mchakato ulio bora wa kuomba hifadhi na kuwekwa kizuizini, ripoti mpya imesema.

Mapema mwaka huu, waliyoomba hifadhi kutoka barani Afrika huko Israel walifanya maandamano makubwa kulalamikia namna wanavyochukuliwa.

Israel ilisema sera zake kwa wahamiaji waliopo kinyume cha sheria na wakimbizi zinaendana na sheria za kimataifa.

Nchi hiyo inasistiza Waafrika si waombaji hifadhi lakini wahamiaji wa kiuchumi wanaoona Israel kama mahala panapovutia kwasababu ni nchi iliyoendelea iliyo karibu wanapoweza kutafuta ajira.

Chanzo: BBC
Imetafsiriwa na Mwandishi wetu







No comments:

Post a Comment