Monday 22 September 2014

MBINU YA KUZUIA EBOLA YAFANIKIWA, SIERRA LEONE

A man travels along a street in his wheelchair during a three-day lockdown to prevent the spread of the Ebola virus in Freetown, Sierra Leone, Sunday, Sept. 21, 2014
Mitaa ya Freetown ilikuwa haina watu kabisa wakati wa amri ya kutotoka nje ilipotolewa

Amri ya kutotoka kwa siku tatu kwa nia ya kuzuia kuenea kwa mlipuko wa Ebola nchini Sierra Leone imetangazwa kufanikiwa na serikali.

Amri hiyo ilisitishwa usiku wa Jumapili na haitosogezwa, serikali ya nchi hiyo imesema.

Sierra Leone ni miongoni mwa nchi zilizoathirika zaidi na mlipuko huo, huku zaidi ya waathirika 550 miongoni mwa 2,600 kwa jumla wakiwa wameripotiwa kuathirika.

Wakati huohuo, nchi jirani ya Liberia imetangaza kuongeza vitanda kwa wagonjwa hao wa Ebola.

Liberia ndio nchi iliyoathirika zaidi na ugonjwa huo, ikiwa zaidi ya nusu ya idadi ya wote waliofariki dunia kutokana na ugonjwa huo wakitoka nchini humo.

Mlipuko wa Ebola Afrika magharibi ni mbaya kuwahi kutokea eneo hilo, Shirika la Afya duniani WHO limesema. Kirusi cha ugonjwa huo huenezwa kwa jasho, damu na mate, na hakuna tiba iliyothibitishwa hadi sasa.

Chanzo: BBC
Imetafsiriwa na Mwandishi wetu

No comments:

Post a Comment