Sunday 21 September 2014

MWAKA SASA SHAMBULIO LA WESTGATE, KENYA

One of the Westgate attackers - September 2013
Picha za CCTV zikionyesha mtu mwenye silaha akisaka watu wa kuwashambulia

Kenya inaadhimisha mwaka tangu shambulio kutokea kwenye eneo la biashara la Westagate, ambapo takriban watu 67 waliuawa.

Kutazinduliwa ishara maalum ya kumbukumbu na maombi maalum huku mishumaa ikiwashwa itafanyika.

Shambulio hilo la Westgate lilidumu kwa siku nne, huku kamera za CCTV zikonyesha wateja wa eneo hilo maarufu la kisasa wenye hofu kubwa wakiwakimbia watu wenye silaha na wengine wakijificha.

Kundi la kisomali la al-Shabab lilisema lilifanya shambulio hilo kufuatia harakati za kijeshi zinazofanywa Kenya nchini Somalia.

Tahadhari kubwa

Siku ya Jumapili, ndugu wa waathirika wataweka mashada katika bustani palipo miti 67 yaliyopandishwa baada ya shambulio hilo.

Dua kutoka imani mbalimbali nazo zitasomwa eneo hilo.

"Tunatarajia familia na marafiki wa waliopoteza ndugu zao kujitokeza na kuwa sehemu ya mchakato huu," Rajes Shah alieyandaa shughuli hiyo alinukuliwa na shirika la habari la AFP.

Siku chache kabla ya kumbukumbu hizi, Kenya iliwekwa katika tahadhari kubwa kwa hofu ya uwezekano wa kuwepo mashambulio mengine na wapiganaji.


No comments:

Post a Comment