Monday 8 September 2014

'KUPIMWA NGUVU' KABLA YA NDOA



Pendekezo la Mahakama Kuu ya Madras kuwataka wanaume na wanawake kufanya vipimo kabla ya kufunga ndoa limewafurahisha wengi huko kusini mwa India na la kushangaza wanawake wengi wameridhishwa na uamuzi huo kuliko wanaume.

"Watoto wa kike mpaka leo wanaonekana kama mzigo usio na umuhimu. Bila hata uchunguzi wa kutosha wa bwana harusi, binti hutolewa kwenye familia zao kwa minajil ya ndoa," Justice N Kirubakaran ameshuhudia katika kesi moja ambapo mwanamke anadai talaka kwa madai kuwa mumewe hana nguvu za kiume.

Uamuzi huo wa mahakama pia umewafurahisha wanasheria, watabibu na jumuiya ya wanafunzi.

Mwanasheria T S R Venkataramana alisema, “Pendekezo la mahakama ni sahihi na ni mabadiliko chanya. Lakini katika hali ya uhalisia haliwezekani. Jamii yetu lazima ibadilike kulikubali hilo.”

Dr Abdul Latiff alisema, “Siku hizi, watoto wa kike na wa kiume wana taarifa nyingi za ngono, ambazo wanajifunza kupitia televisheni na mtandao. Hivyo vipimo kabla ya ndoa ni jambo jema.

Hata hivyo, alisema si rahisi kutekeleza. Miaka kadhaa iliyopita, kuonyesha cheti cha hospitali cha kupima ukimwi kabla ya ndoa ilisistizwa, hata hivyo, lengo halikufanikiwa.

Chanzo: The Times of India

1 comment:

  1. kweli ni bora kujua nini na vipi ndoa yenu itakavyokuwa

    ReplyDelete