Saturday 20 September 2014

SARKOZY ATANGAZA KUREJEA SIASA ZA UFARANSA

 

Aliyekuwa Rais wa Ufaransa Nicolas Sarkozy ametangaza kurejea katika siasa.

Katika ukurasa wake wa Facebook, alisema atagombea uongozi wa chama cha upinzani UMP, ikionekana zaidi kama hatua moja mbele katika kugombea urais mwaka 2017.

"Mimi ni mgombea wa kuwa Rais wa familia yangu ya kisiasa," Bw sarkozy aliandika.

Taarifa hiyo inatuliza miezi ya hisia juu ya nia ya mgombea huyo mwenye umri wa miaka 59 wa chama cha Conservative, ambaye aliapa kuacha siasa baada ya kushindwa kuchaguliwa upya nafasi ya urais mwaka 2012.

Uchaguzi wa chama cha UMP unatarajiwa kufanyika mwezi Novemba.


No comments:

Post a Comment