Sunday 14 September 2014

RAIS AWAFUKUZA MAAFISA 'WALIOONDOKA' LIBERIA

Food delivered in Monrovia, 12 Sept
Chakula cha msaada chagaiwa kwa maelfu ya walioathirika na Ebola, Liberia

Rais wa Liberia Ellen Johnson Sirleaf amewafukuza kazi maafisa wa serikali 10 walio "nje ya nchi bila sababu yoyote", huku nchi hiyo ikiwa ina mgogoro wa taifa wa Ebola.

Alisema maafisa hao wameonyesha "kutojali janga letu la taifa na kuipiuuza serikali".

Viongozi hao walipewa makataa ya wiki moja zaidi ya mwezi mmoja uliopita warejee nyumbani.

Sierra Leone, Liberia na Guinea ni nchi zilizoathiriwa zaidi katika mlipuko wa ugonjwa huo uliouwa zaidi ya watu 2,400.

Zaidi ya nusu waliofariki dunia kutokana na virusi vya Ebola walikuwa Liberia.

Maafisa hao 10 ni pamoja na makamishna wawili, wasaidizi sita wa mawaziri na manaibu waziri wawili katika wizara ya sheria, Wheatonia Dixon-Barns na Victoria Sherman-Lang.

Maafisa wengine wanane nao wamepewa onyo kurejea nchini humo, na hawatolipwa mpaka warudi.

No comments:

Post a Comment