Thursday 11 September 2014

MARUFUKU KUMWITA MWANAO 'MESSI'



Lionel Messi with his partner and son (Reuters)
Lionel Messi akiwa na mpenzi wake na mwanawe
Wazazi wanaotaka kuwaita watoto wao wa kiume jina kama la mchezaji nyota wa Barcelona Lionel Messi sasa watakatazwa kufanywa hivyo katika eneo alipozaliwa mchezaji huo.

Serikali ya Argentina imeamua kuzuia watoto wengine zaidi kuitwa ‘Messi’ kwa madai kuwa hali imevuka mipaka.

Hayo yote yameibuka baada ya Hector Varela kutoka Rio Negro kusini mwa Argentina alipopambana na mamlaka ili kuruhusiwa kumwita mtoto wake wa kiume Messi Daniel Varela.

Hili lilikuwa tukio la kwanza la namna hiyo kutokea nchini humo

Kulingana na gazeti la Hispania Marca, mkurugenzi wa usajili wa majina katika jimbo la Santa Fe, Gonzallo Carrillo, alisema Messi kwa sasa limepigwa marufuku kutumika kama jina la mwanzo.

Sasa ni “kinyume cha sheria”, lilisema gazeti hilo, katika njia ya kuondosha mchanganyiko.

Kuhusu jina la mwanawe, Varela alisema: “Mimi ni baba yake Messi. Watu wengi wamewapa watoto wao wa kiume jina la Lionel wakimaanisha Messi, lakini hili liko wazi zaidi”.

Aliomba ruhusa maalum kutoka serikalini, bila kujua kuwa mwanawe alikuwa ndio wa kwanza Argentina na lingeleta vurumai.

Hatimaye, mwanawe wa kiume alifanikiwa kusajiliwa kama “Messi Daniel Varela'.

Mapema mwaka huu, taasisi ya kuwashughulikia wanyama Catalonia ilitoa takwimu zilizopendekeza kuwa paka na mbwa 701 eneo hilo wamepewa majina ya nyota huyo wa soka.

Chanzo: yahoo sport
Imetafsiriwa na Mwandishi wetu

No comments:

Post a Comment