Friday 12 September 2014

OSCAR PISTORIUS AKUTWA NA HATIA



 
Mwanariadha wa Afrika Kusini Oscar Pistorius amekutwa na hatia kwa kosa la kuua bila kukusudia (Culpable homicide) baada ya jaji kuona amemwuua mpenzi wake kwa bahati mbaya.

Jaji Thokozile Masipa amesema alikuwa “mzembe” alipofyatua risasi iliyopitia mlango wa chooni lakini akiwa “anaamini kulikuwa na mtu asiyemjua”.

Alisema upande wa mashtaka umeshindwa kuthibitisha kuwa alikuwa na nia ya kumwuua Reeva Steenkamp.

Pia alikutwa na hatia ya kushikilia silaha kwa uzembe iliyofyatuka kwenye mgahawa

Mwandishi wa BBC Andrew Harding, akiwa mahakamani, alisema kufuatia uamuzi huo, Pistorius alikaa tu, akafuta uso wake na kusogea kidogo kwa mbele.

Hakukuwa na hisia zozote mahakamani kwasababu kila mmoja alijua uamuzi gani ungetolewa, mwandishi huyo aliongeza.

Uamuzi huo unaashiria mshtakiwa huyo atakabiliwa na kifungo cha mpaka miaka 15, japo wataalamu wa kisheria wanasema huenda ikawa miaka saba hadi kumi baada ya hukumu kutolewa katika wiki chache zijazo.

No comments:

Post a Comment