Wednesday 10 September 2014

WATANZANIA 2 NA WANYARWANDA 2 WAFUNGWA AFRIKA KUSINI


Gen Faustin Kayumba Nyamwasa in court in Kagiso near Krugersdorp on 28 August 2014
Jenerali Nyamwasa ameilaumu serikali ya Rwanda kuhusika na ufyatuliaji risasi

 Mahakama ya Afrika kusini imewahukumu watu wanne kufungwa miaka nane jela kwa kosa la jaribio la kumwuua aliyekuwa mkuu wa majeshi wa Rwanda Jenerali Faustin Kayumba Nyamwasa.

Alipigwa risasi tumboni mjini Johannesburg Juni 2010, siku chache baada ya kukimbia Rwanda baada ya mfarakano na Rais Paul Kagame.

Hakimu mkazi alisema “watuhumiwa wakuu” hawajakamatwa.

Mashambulio kadhaa dhidi ya waombaji hifadhi wa Rwanda nchini Afrika kusini yamesababaisha mvutano wa kidiplomasia baina ya Pretoria na Kigali.

Serikali ya Rwanda imekana kabisa kuhusika na mauaji ya wapinzani wake Afrika Kusini.

'Bado wana woga '

Upande wa mwendesha mashtaka ulitaka wapewe kifungo cha miaka 15 kwa Wanyarwanda wawili, Amani Uriwane na Sady Abdou, na Watanzania wawili Hassan Mohammedi Nduli na Hemedi Dendengo Sefu,waliotiwa hatiani kwa jaribio la mauaji.

Kuwapa kifungo cha miaka minane kila mmoja, Hakimu Stanley Mkhari alisema kuwa watu hao walikuwa kizuizini tangu tukio hilo la ufyatuaji risasi kutokea.

"Nyie si watuhumiwa wakuu katika suala hili. Kwa maoni yangu mlitakiwa kuwa mbele yangu na wote waliowezesha pesa kupatikana na waliowafadhili kufanya uhalifu huo," amenukuliwa akisema.

Wanaume wengine wawili waliachiwa huru kwa kuhusishwa na kosa hilo mwezi uliopita.

Jenerali Nyamwasa alisema alikuwa amefurahi baada ya kutolewa uamuzi wa hukumu hiyo, lakini bado ana wasiwasi na usalama wa Wanyarwanda waishio uhamishoni, shirika la habari la Reuters limesema.

 

No comments:

Post a Comment