Tuesday 9 September 2014

MTOTO WA OBASANJO APIGWA RISASI, NIGERIA



Former President Olusegun Obasanjo (March 20110
Aliyekuwa Rais Olusegun Obasanjo alipigana katika vita vya wenyewe kwa wenyewe Nigeria 1967-1970
Mtoto wa kiume wa aliyekuwa Rais wa Nigeria Olusegun Obasanjo amepigwa risasi na kujeruhiwa katika mapambano na wapiganaji, msaidizi wa Bw Obasanjo  alisema.

Lt  Kanali Adeboye Obasanjo  alijeruhiwa wakati  jeshi  lilipojaribu kudhibiti upya miji kaskazini-mashariki mwa jimbo la Adamawa kutoka kwa Boko Haram, Muhammad Keffi ameiambia BBC.

“Idadi kubwa ya wapiganaji” pia waliuawa katika mapambano hayo, jeshi lilisema.

Mwezi uliopita, Boko Haram walitangaza kuwepo na taifa la Kiislamu katika maeneo wanayodhibiti kaskazini-mashariki mwa Nigeria.

Wataalamu walionyesha wasiwasi kuwa Nigeria, nchi yenye idadi ya watu wengi zaidi barani Afrika, inaweza kugawanyika kama ilivyo Iraq na Syria ambapo kundi la wapiganaji la IS limetangaza kuwa Taifa la Kiislamu.

Wapiganaji wa Boko Haram wameteka Michika na Bazza, miji miwili karibu na mji ulio maarufu kibiashara wa Mubi, katika siku za hivi karibuni.

No comments:

Post a Comment