Monday 22 September 2014

RAIS MUSEVENI KUWEKEWA VIZINGITI NA WAPENZI WA JINSIA MOJA, MAREKANI

Rais Yoweri Museveni wa Uganda

Kundi la wapenzi wa jinsia moja Dallas, Texas, Jumatano iliyopita walizilamisha hoteli mbili kumkatalia Rais Museveni kukaa, kwa madai kuwa ni mkiukaji wa haki za binadamu.

Kulingana na wavuti ya haki za wapenzi wa jinsia moja dallasvoice.com, Rais alishapanga kufikia hoteli ya Four Seasons huko Irving na baada pia ya kupanga Raylard Texan Resort na Convention Center napo alikataliwa baada wapenzi hao inavyodaiwa kupiga simu chungu nzima, wakitaka hoteli hizo zisimpokee.

"Watu wangu walinipangia hoteli, lakini hawa wapenzi wa jinsia moja wamezuia. Nikasema waambie hao watu walionialika kunitafutia sehemu ya kulala. Sio kwamba nina usongo wa kuja Texas." Bi Sarah Kagingo, msaidizi maalum wa Museveni anayesimamia mitandao yake ya kijamii alimnukuu Rais huyo kwenye taarifa iliyotolewa.

Hatahivyo, kulingana na Bi Kagingo, Rais huyo baadae alipangiwa hoteli nyingine - Howdy Lone Star Ranch huko Texas.

Bw Museveni alikuwa akikutana na Waganda waishio nchi za nje siku ya Jumapili, Texas kujadili uwezekano wa kuwekeza na kuchangia katika ukuaji wa kiuchumi Uganda.

Rais huyo aliwahakikishia wawekezaji kuwa ameandaa mpango kupitia nyanja mbalimbali kurahisisha uwekezaji nchini humo.

Chanzo: Daily Monitor, Uganda
Imetafsiriwa na Mwandishi wetu


No comments:

Post a Comment