Monday 8 September 2014

BUNGE LA IRAQ LAAPISHA SERIKALI YA UMOJA



The new Iraqi government is seen during a swearing in ceremony in Baghdad, Iraq, 8 September 2014
Wanachama wengi wa bunge hili jipya waliapishwa siku ya Jumatatu

Bunge la Iraq limepitisha serikali mpya ikiwa na manaibu waziri mkuu wa Ki-Sunni na Ki-Kurdi, huku ikijaribu kupambana na wapiganaji wa IS waliodhibiti maeneo mengi ya nchi hiyo.

Saleh al-Mutlak na Hoshyar Zebari wamepitishwa ndani ya makubaliano ya kugawana madaraka baada ya wiki mbili za mfarakano wa kisiasa.

Waziri mkuu Haidar al-Abadi, Mshia mwenye msimamo wa kati, aliombwa kuunda serikali baada ya kujiuzulu kwa Nouri Maliki.

Hata hivyo, hawajakubaliana kuhusu waziri wa ndani na wa ulinzi.

Bw Abadi ameahidi kujaza nafasi hizo katika kipindi cha wiki moja.

Mrithi wake alilazimishwa kujiuzulu mwezi Agosti, kufuatia Waarabu wa Kisunni na jumuiya za Kikurdi kushutumu serikali yake kuweka sera za upinzani.

Marekani iliisihi Iraq kuunda serikali itakayohusisha wote wakiwemo wawakilishi wa Sunni, wakiielezea kama sharti la kuongeza nguvu za kijeshi dhidi ya IS.


Chanzo: BBC
Imetafsiriwa na Mwandishi wetu








No comments:

Post a Comment