Sunday 28 September 2014

NYOTA WA FILAMU GEORGE CLOONEY AFUNGA NDOA



George Clooney and his fiancee Amal Alamuddin arrive in Venice, 26 September

Nyota muigizaji wa Hollywood George Clooney amemwoa mwanasheria wa kutetea haki za binadamu  Amal Alamuddin huko Venice, miongoni mwa matukio yaliyokuwa yakisubiriwa kwa hamu zote.

Wenzake ambao ni maarufu pia kwenye tasnia ya uigizaji na uimbaji katika mji wa Italia walimiminika kushuhudia muungano huo wa kapera maarufu katika uwanda wa filamu, mwenye umri wa miaka 53, na Bi Alamuddin, mwenye umri wa miaka 36.

Shughuli hiyo ilisherehekewa katika hoteli iliyoelekea kwenye mfereji mkubwa wa Venice.

Wakala wa Clooney walitoa taarifa hiyo kwa waandishi wa habari.

Kulingana na shirika la habari la AP, hiyo ndio itakuwa taarifa pekee itakayotolewa kuhusu harusi hiyo.




No comments:

Post a Comment